The House of Favourite Newspapers

Rais Samia Atembelea Kwenye Kaburi la Rais wa Kwanza wa Malawi – Video

0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiweka shada la maua kwenye kaburi la Rais wa Kwanza wa Malawi na Baba wa Taifa hilo Hayati Dkt. Kamuzu Banda lililopo katika Makumbusho ya Kamuzu, Lilongwe nchini Malawi tarehe 6 Julai, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ameendelea na ziara yake huko nchini Malawi ambapo hii leo ametembelea na kuweka shada la maua kwenye kaburi la Rais wa Kwanza wa Malawi na Baba wa Taifa hilo Hayati Dkt. Kamuzu Banda lililopo katika Makumbusho ya Kamuzu, Lilongwe nchini humo ambapo wakati akitoka kwenye makumbusho hayo alikutana na kusalimiana na Mama Cecilia Kadzamira ambaye alifanya kazi kwa karibu na Rais wa Kwanza wa Malawi na Baba wa Taifa hilo Hayati Dkt. Kamuzu Banda.

Rais Samia akipanda mti nje ya Ofisi za Bunge la Malawi kama kumbukumbu wakati alipofanya ziara Ofisini hapo Jijini Lilongwe nchini Malawi tarehe 6 Julai, 2023.

Pia, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amepanda mti nje ya Ofisi za Bunge la Malawi kama kumbukumbu wakati alipofanya ziara Ofisini hapo Jijini ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa ziara yake iliyoanza hapo jana nchini Malawi.

Aidha, Rais Samia Suluhu bado yupo nchini Malawi akiendelea na ziara yake hiyo kufuatia mwaliko kutoka kwa mwenyeji wake, Rais wa Malawi, Lazarus Chakwera kuhudhuria maadhimisho ya miaka 59 ya uhuru wan chi hiyo ya Malawi.

Rais Samia Suluhu akisalimiana na Mama Cecilia Kadzamira ambaye alifanya kazi kwa karibu na Rais wa Kwanza wa Malawi na Baba wa Taifa hilo Hayati Dkt. Kamuzu Banda wakati alipokuwa akitoka kwenye Makumbusho ya Kamuzu, Lilongwe nchini Malawi tarehe 6 Julai, 2023.
Rais Samia Suluhu Hassan akisaini Kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili kwenye Ofisi za Bunge la Malawi zilizopo Jijini Lilongwe tarehe 6 Julai, 2023. Kulia ni Makamu wa Rais wa Malawi Dkt. Saulos Klaus Chilima akiwa pamoja na Spika wa Bunge hilo Bi. Fiona Kalemba kushoto.

PICHA NA IKULU

Leave A Reply