The House of Favourite Newspapers
gunners X

Rais Samia Azindua Majengo ya Taasisi ya Sayansi za Bahari Zanzibar (Picha +Video)

0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na viongozi mbalimbali mara baada ya kuwasili katika Jengo la Taaluma na Utawala la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Taasisi ya Sayansi za Bahari, Buyu Zanzibar.

ZANZIBAR – Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, amezindua rasmi majengo mapya ya Taasisi ya Sayansi za Bahari (UDSM – IMS) Zanzibar, akisisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya wahadhiri, watafiti, sekta binafsi, taasisi za serikali na jamii kwa ujumla.

“Ninawahimiza wahadhiri na watafiti kuimarisha ushirikiano na sekta binafsi, taasisi za serikali na jamii kwa ujumla ili tafiti hizi zinazofanyika hapa ziwe na matokeo ya moja kwa moja kwa maendeleo ya wananchi,” alisema Rais Samia katika hafla hiyo.

Taaissi hii, iliyoko chini ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ina lengo la kukuza utafiti wa kisayansi katika masuala ya bahari, ikiwemo uhifadhi wa rasilimali za baharini, uvuvi endelevu, na maendeleo ya jamii zinazotegemea bahari. Rais Samia alibainisha kuwa matokeo ya tafiti haya yanapaswa kuleta faida halisi kwa wananchi wa Zanzibar na taifa kwa ujumla.

Rais Samia akivuta kitambaa pamoja na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kama ishara ya uzinduzi wa Jengo la Taaluma na Utawala na Bweni la Wanafunzi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Taasisi ya Sayansi za Bahari, Buyu Zanzibar.
Rais Samia akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Jengo la Taaluma na Utawala na Bweni la Wanafunzi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Taasisi ya Sayansi za Bahari, Buyu Zanzibar.
Taswira ya Jengo la Taaluma na Utawala na Bweni la Wanafunzi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Taasisi ya Sayansi za Bahari, Buyu Zanzibar mara baada ya kuzinduliwa na Rais  Samia Suluhu Hassan, Buyu Zanzibar.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Profesa Adolf Mkenda kwenye picha ya pamoja na viongozi mbalimbali mara baada ya kuzindua Jengo la Taaluma na Utawala na Bweni la Wanafunzi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Taasisi ya Sayansi za Bahari, Buyu Zanzibar tarehe 08 Januari, 2026.

Leave A Reply