The House of Favourite Newspapers

Bia Ya Kopo Ya Safari Lager 500ml Yaendelea Kubamba Kitaa

Bila shaka umeshaliona tangazo hili matata kabisa la Safari Lager ukipita Barabara ya Kawawa jijini Dar, wajanja wanakwambia utaalamu uliotumia kutengeneza bango hilo la 3D ni wa hali ya juu sana. 
Tangazo hili limekuwa likiwavutia wapita njia katika barabarani hiyo na kuwateka hisia zao, “Dah yaani hili tangazo tu lilivyo linakufanya uitafute bia yenyewe uishushe kinywani” alisikika mmoja wa muenda kwa miguu.
 
Sasa si tu kwamba tangazo linateka hisia na kuwa kivutio, bia yenyewe ina ladha nzuri ya aina yake na inaleta urahisi na unafuu kwa mtumiaji yeyote wa Safari Lager. Kampuni ya Bia ya TBL ilizindua bia hii ya kopo ya kwanza yenye ujazo wa mililita 500 kwa bia ya Kitanzania mwishoni mwa mwezi wa 8 mwaka huu na hadi sasa imeonekana kuwa kipenzi cha watumiaji katika maeneo mbalimbali nchini.
 
“Bia mpya ya kopo ya Safari ni dhahiri kwamba imetengezwa kumpa umahiri Mtanzania katika safari ya maisha yake. Inapatikana kwa urahisi na kwa wakati muafaka hata wakati mtu anakwenda kwenye mihangaiko yake au kubeba akiwa anakwenda kwenye matembezi au safarini” alisema Meneja Bidhaa wa Safari Lager, Edith Bebwa
Meneja Bidhaa wa Safari Lager, Edith Bebwa alipokuwa akitambulisha bia mpya ya Safari Lager kwenye kopo la mililita 500 ambayo inapatikana Tanzania nzima.
Baadhi ya wateja wakiwa na nyuso za furaha baada ya kujipatia bia mpya ya Safari Lager katika kopo lenye ujazo wa 500ml

Comments are closed.