Diamond Aibuka na Majina 7 kwa Mtoto Wake Mchanga Aliyezaliwa Leo, Aomba Mashabiki Wamchagulie Moja
Pretoria, Afrika Kusini: BAADA ya taarifa kusambaa kwenye social media kuwa msanii wa Bongo Fleva hapa nchini, Nasbu Abdul “Diamond Platnumz” leo leo Desemba 6, 2016, mpenzi wake Zarina Hassan “Zari The Boss Lady” amejifungua mtoto wa kiume katika Hospitali ya Netcare iliyopo mjini Pretoria nchini Afrika Kusini.
Diamond aliyekuwa akihaha kutafuta jina gani atampa mwanaye huyo huku akisema kuwa amewaachia wanafamilia wakubaliane, hatimaye ameibuka na kuorodhesha majina saba kwenye akaunti yake ya instagram ambayo ameomba mashabiki wamsaidie kuchagua jina lipi linafaa kumuita mwanaye huyo.
Ameandika hivi:
Help me to Pick One for my Baby Boy Please….. RAMIA….NILLAN… LANIER…. AKRAM RAHUL…RIAZ….. DYLAN…?
Comments are closed.