The House of Favourite Newspapers

Irene Paul Atoa Somo la Matumizi Ya Kemikali

0
Irene Paul

MUIGIZAJI mzuri anapokuwa mbele ya kamera,Irene Paul amehamasisha mastaa na watu mbalimbali kuepuka gharama ya kujipodoa kwa kemikali za dukani kwani nyingi zina madhara, badala yake wanaweza kubaki na uasili wao na wakapendeza zaidi.

 

Akizungumza na gazeti hili Irene alisema, amekaa na kujitathimini yeye mwenyewe ambapo hatumii gharama ya kununua nywele za bei au kutumia madawa ya usoni lakini anaonekana mrembo sana na kuona ni vyema atoe somo hilo kwa watu wengine.

 

“Ukitaka kuniangalia kuanzia kichwani mpaka ngozi yangu situmii gharama hata kidogo kwenye mwili wangu na ninatumaini hata mastaa wengine wakiamua kuwa jinsi walivyo watapendeza na wataepuka gharama ambazo si za muhimu ,” alisema Irene.

Leave A Reply