The House of Favourite Newspapers

Shamsa Awachana Mastaa Wenzake!

Staa wa filamu za Kibongo, Shamsa Ford.

 

STAA wa filamu za Kibongo, Shamsa Ford amefunguka kuwa mastaa wengi wanachagua watu wa kuwaoa huku wengi wakiwa na ndoto za kuolewa na matajiri jambo ambalo si sahihi.

 

Akizungumza na gazeti hili bila kuwataja majina Shamsa alisema, mastaa wengi wamejisahau sana kuwa maisha yamebadilika kikubwa ni kila mtu amuangalie aliyenaye ni mtu mwenye msimamo gani maishani.

 

“Mastaa wengi wanakosea pale wanapofikiria kuwa wao wanatakiwa waolewe na watu wenye fedha na uwezo mkubwa kimaisha, wanakosea kabisa. Sivyo inavyotakiwa, kikubwa kumuangalia mtu ana msimamo gani na kuweka ustaa pembeni, ” Alisema Shama.

STORI NA IMELDA MTEMA | AMANI – GPL

Comments are closed.