The House of Favourite Newspapers

Sharon Williams Aibuka Mshindi wa Miss IFM 2018/19

Mshindi wa Miss IFM, Sharon Williams, akionyesha cheti chake baada ya kuibuka mshindi wa chuo hicho ambapo mashindano yalifanyika katika Ukumbi wa King Solomon, jijini Dar es Salaam, usiku wa kuamkia leo.
Hawa ndio walioingia ‘Top 5’ ambao kutoka kushoto ni Diria Nasasi aliyekuwa mshindi wa tano, Janeth Richard (mshindi wa pili), Sharon Williams, Mary Jeremia (wa tatu) na Esther Huruwe (wa nne).
Majaji wa shindano hilo la IFM wakiongozwa na Hamisa Mobetto (wa pili kutoka kushoto) na jaji mkuu Martin Kadinda (kulia).
Mwanamitindo na mzazi mwenziye mwanamuziki Diamond Platnumz, Hamisa Mobetto, akiwa katika pozi wakati wa shindano hilo.

SHINDANO la kumpata mrembo kutoka Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) lilifanyika usiku wa kuamkia leo katika Ukumbi wa King Solomon, jijini Dar es Salaam, na mshindi alikuwa Sharon Williams  aliyezawadiwa sh. 800,000, wa pili alipata 500,000, wa tatu 300,000 na waliobaki walizawadiwa 100,000.

Comments are closed.