The House of Favourite Newspapers

Wachezaji Yanga Waache Mzaha, Tupeni Raha Leo

NIWAPONGEZE Simba ambao kwa msimu huu wame­fanikiwa kutwaa ub­ingwa wa Ligi Kuu Bara baada ya kuonyesha juhudi ya hali ya juu tangu kuanza kwa ligi, lakini pongezi zangu za dhati ziende kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kutokana na kufanikiwa kwa kiasi fulani katika usimamizi wa ligi zetu za ndani.

 

Licha ya misuguano na changamoto za hapa na pale ambazo ni ngumu wakati mwingine kuziepuka kutokana na miundombinu ya nchi yetu ingawa naamini huu ni mwanzo tu wa kuelekea katika mabadi­liko makubwa ya kimipango ka­tika soka letu.

 

Lakini ukiondoa ubingwa wa Simba ambao bado wamebaki­wa na mechi mbili za kukamili­sha mechi 30 za Ligi Kuu Bara wakiwa sawa na Azam ambao wanashika nafasi ya pili wakiwa na pointi 52 wakifutia na Yanga ambao wanakamata nafasi ya tatu na pointi zao 48 huku wak­iwa na mechi nne mkononi.

Kwa sasa vita ya ubingwa imeshafikia ukingoni baada ya Simba kufanikiwa kutwaa wakiwa na pointi 68 isipokuwa vita kubwa ipo kwa upande wa Azam na Yanga katika kugo­mbania nafasi ya pili ingawa Yanga wana nafasi kubwa ya kuweza kuichukua kutokana na idadi ya mechi waliobakiwanazo tofauti na Azam ambao wana mechi mbili pekee.

 

Naamini hapa lazima patachimbika kwa timu hizo kuhakikisha wanafanya vizuri katika mechi zilizobakia ili ku­weza kupata nafasi hiyo ingawa haitaweza kusaidia kushiriki michuano ya kimataifa msimu ujao kwa kuwa mshiriki wake anatoka kwenye Kombe la FA.

 

Upande mwingine tumeweza kuishuhudia timu yetu ya taifa ya vijana chini ya miaka 20, Ngorongoro Heroes ikishindwa kupata matokeo ya ushindi ka­tika mchezo wake wa kuwania kufuzu fainali za vijana zitaka­zofanyika Niger baada ya ku­fungwa mabao 2-1 na Mali.

 

Matokeo hayo, binafsi naamini hayakustahili kupata timu yetu ya vijana kwa kuwa walikuwa kwenye uwanja wa nyumbani lakini ndani yake uki­angalia kwa makini unaona timu yenyewe inakosa muunganiko wa kutosha licha ya mwalimu wake Ammy Ninje kuwa na maneno mengi lakini upande wa vitendo bado shida.

 

Ngorongoro hawakustahili kufungwa na Mali kwa kuwa Mali hawa ndiyo ilikutana na Serengeti Boys katika michuano ya vijana kule Gabon na hata kama kuna mabadiliko yaliofan­yika basi yalikuwa machache kwa upande wa Mali na Ngorongoro k w a n i w a c h e z a j i wao wali­p a n d i s hwa madaraja.

 

L a k i n i k u t o k a n a na mipango mibaya ya m w a l i m u , timu ilishindwa kupata ushindi ingawa tunaweza kwenda ku­fanya vizuri kwao iwapo benchi la ufundi litafanya maamuzi sa­hihi.

 

Nikiachana na hayo, leo Ju­matano wawakilishi wa Tan­zania katika mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika, Yan­ga, watacheza mechi yao ya pili katika Kundi D, dhidi ya Rayon Sport kutoka nchini Rwanda huku ikiwa imeshapoteza mch­ezo wa kwanza dhidi ya USM Alger.

Katika mchezo huo utakao­pigwa saa moja usiku kwenye Uwanja wa Taifa, Dar, Yanga ina­paswa kupambana na kuhakikisha inapata ushindi ili kuweza kuji­wekea mazingira mazuri kwa kuwa ukiangalia mpaka sasa hakuna timu ambayo ina nafa­si kwenda hatua ya robo fainali ikiwemo Gor Ma­hia kutoka kundi hilo.

 

Kweli hakuna asiyejua kwamba Yanga ipo katika hali mbaya ya kiuchumi lakini hii isiwe sababu ya wao kushindwa kufanya vizuri kwa kuwa ushindi watakaoweza kupata leo ndiyo pesa yenyewe itakayoweza ku­walipa wao.

 

Niwaambie wachezaji haya masuala ya timu kukosa fedha za kulipa wachezaji hata wakati wetu yalikuwepo lakini kikubwa wachezaji tulikuwa tukiangalia na maslahi ya timu zetu, yaani nini inachokihitaji ili kuweza ku­fikia malengo na kwa nini wakati wenu liwe tatizo ambalo wen­gine linasababisha kugomea kucheza.

 

Binafsi naona huu ndiyo wakati wa wachezaji kuunga­na kwa kupata ushindi wakati masuala yenu yanafanyiwa kazi kwa kuhakikisha Rayon anafun­gwa kwenye Uwanja wa Taifa kwa kuwa ukubwa na thamani ya mashindano haya ni kuwa na sehemu ya kuweza kujiuza kama mchezaji na siyo kufanya michezo ya kugomea.

UCHAMBUZI: Mohammed Hussein

Comments are closed.