The House of Favourite Newspapers

Samsal Mabingwa Soka La Ufukweni Jjijini Dar

Baadhi ya Wachezaji wa Samsal Mikocheji wakishangilia na Kikombe pamoja na hundi ya shilingi milioni moja mara baada ya kuibuka mabingwa katika mashindano ya Soka la ufukweni yaliyomalizika mwishoni mwa wiki katika ufukwe wa Coco Beach jijini Dar es Salaam.

 

TIMU ya Samsal yenye makazi yake Mikocheni jijini Dar es Salaam wameibuka mabingwa katika mashindino ya Soka la ufukweni lililomalizika mwishoni mwa wiki na hivyo kuzawadia kikombe pamoja na hundi ya Shilingi milioni moja.

 

Samsal waliibuka mabingwa baada ya kuifunga timu ya Safina yenye makazi yake Ukonga jijini Dar es Salaam 3-2, na kwa matokeo hayo nafasi ya pili ilichukuliwa na timu ya Safina na hivyo kuzawadiwa pesa taslimu Shilingi laki sita(600,000/=).

Baadhi ya Wachezaji wa Samsal wakimpongeza Kocha wao kwa kumrusha juu mara baada ya kuibuka mabingwa katika mashindano ya Soka la ufukweni yaliyomalizika mwishoni mwa wiki katika ufukwe wa Coco Beach jijini Dar es Salaam.Timu hiyo ilizawadiwa Kikombe na hundi ya shilingi milioni moja.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mkurugenzi wa Verge Africa, Rajan Kumar ambao ndio waratibu alisema mashindano haya yalianza na Kampeni ya kufanya usafi Ufukwe wa Coco Beach kwa kushirikisha Wafanyakazu wa makampuni ya Pepsi, RedBull, Slipway Hoteli, G1 Security Limited, AfyaPal (Muhimbili), Toshiba, Zenufa, HasafaScience, Verge Africa na Nipe Fagio juni 15,2019 na baadae pakafuatiwa mashindano ya soka la ufukweni ambalo limemalizika mwishoni mwa wiki hii kwa kushirikisha timu 14 ambazo niDar Beach Warmer, Every Living things, Safina Athletics, Mkude Fc, Osterbay City, JMK Fc, Beach Boys, CBE Combine, Samsal Fc, All Stars, We Kick Balls Fc, GEGE Fc, Gerezani Fc, Future Stars.

 

Kumar aliyashukuru makampuni yote yaliyojitokeza kushiriki Kampeni hiyo pamoja na timu shiriki zote na kuwaomba wasikose kujitokeza tena mwakani.

 

Comments are closed.