The House of Favourite Newspapers

Aunt: Maisha Yamekuwa Magumu

STAA wa filamu za Kibongo, Aunt Ezekiel amefunguka kuwa mastaa wengi akiwemo yeye, wameanza kusahaulika kwenye jamii kutokana na kuhangaika na maisha na kusahau burudani kama ilivyokuwa zamani.

 

Akiteta mbele ya kizimba cha MIKITO, Aunt alisema kasi ya maisha ya sasa inafanya kila mtu apambane na hali yake na kupunguza baadhi ya mambo waliyoyazoea.

 

“Hatuonekani mara kwa mara, wala kusikika siku hizi kwa sababu maisha yamekuwa magumu, ni lazima kujituma zaidi na sio kujionesha au kuubeba umaarufu tu huku maisha yako yanateketea,” alisema Aunt.

Comments are closed.