The House of Favourite Newspapers

BABA, BINTI WAKAMATWA KWA KUDAIWA KUZAA MTOTO

Steven Pladl (kushoto) akiwa na  na binti yake Katie Pladl (20).

STEVEN PLADL (42) wa Knightdale, North Carolina, Marekani, na binti yake Katie Pladl (20) walikamatwa Jauari 27 mwaka huu baada ya mke (mtalaka) wa Pladl, kuripoti polisi kwamba watu hao wawili wamezaa mtoto. Imedaiwa Katie alikuwa amechukuliwa katika vituo vya kulelea watoto na kwenda kulelewa kwengine lakini alipotimiza umri wa miaka 18 aliwagundua wazazi wake wa kweli kupitia mitandao ya kijamii na kwenda kuishi nao Agosti 2016.

Kwa mujibu wa kituo cha televisheni cha KRON4, Steven Pladl na mkewe (hakutajwa jina lake) waliyetengana rasmi Novemba 2016, aliiambia polisi kwamba Steven Pladl alikuwa analala na Katie kabla hawajatengana. Inadaiwa mwanamke huyo aligundua kwamba mwanamme huyo alikuwa amemtia mimba Katie ambapo alikuwa akiwaambia watoto wake kumwita Katie mama yao mdogo.

 

Steven Pladl anadaiwa alikiri kwa mtalaka wake huyo jambo na kwamba alipanga kumwoa binti huyo. Na kwa mujibu wa mtandao wa Instagram, Katie hivi sasa ameolewa lakini haijulikani mtoto wa kiume waliyekuwa naye wakati wanakamtwa yuko chini ya matunzo ya nani. Wawili hao wanashitakiwa kwa makosa ya kujamiiana ndugu kwa ndugu ambapo Steven Pladl yuko nje kwa dhamana na Katie yuko ndani kusubiri kesi iendelee.

Comments are closed.