RAIS wa Chama cha Madaktari nchini, Elisha Osati, amezungumzia suala la kufukuzwa kwa daktari wa Kituo cha Afya Ngarenaro, Dkt. Japhet Kivuyo, mkoani Arusha baada ya kukutwa hayuko kazini ambapo uamuzi wa kufukuzwa kwake ulitolewa na Katibu Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Levelosi.
Dkt. Osati amezungumza na wanahabari leo kuhusu uamuzi huo ambao ume-trendi kwenye mitandao ya kijamii na kuibua maswali mengi kuhusu uhalali wa kiongozi wa kisiasa kumwajibisha mtumishi wa umma.
Comments are closed.