The House of Favourite Newspapers

Taswira ya kuagwa mwili wa, Celina Kombani leo, Dar

0

kombani (2)-001Jaji Mkuu Msitaafu, Joseph Sinde Warioba akichukua nafasi na kuketi.kombani (4)Viongozi mbalimbali wakiwasili Viwanja vya Karimjee jijini Dar, kwa ajili ya kuaga mwili wa marehemu Celina Kombani.kombani (3)Waombolezaji waliofika Viwanja vya Karimjee kuaga mwili wa marehemu Kombani.

kombani (1)-001Bi. Celina Kombani, enzi za uhai wake.
4.Askali wa Bunge wakibeba jeneza la mwili wa ,Celine Kombani mara baada ya kuwasili Uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu, Julius Nyerere jijini Dar.Mwili wa Marehemu Kombani ulivyoshushwa Uwanja wa Ndege wa Mwl. Nyerere kutoka India, juzi.

kombani1Aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Mbunge wa Ulanga Mashariki (CCM), Bi. Celina Kombani.

Mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Mbunge wa Ulanga Mashariki (CCM), Bi. Celina Kombani utaagwa rasmi leo Jumatatu, kuanzia majira ya saa nne asubuhi katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Bunge, baada ya zoezi la kuaga mwili wa marehemu na kutoa heshima za mwisho, utasafirishwa kwenda mkoani Morogoro kuanzia majira ya saa tisa alasiri ambapo utalala nyumbani kwake Forest Hill.

Jumanne kuanzia majira ya saa nne asubuhi, itafanyika ibada maalum ya mazishi na baadaye mwili utaagwa katika Viwanja vya Jamhuri mjini Morogoro na kufuatiwa na mazishi shambani kwake, Lukobe nje kidogo ya mji wa Morogoro.

Live Updates kutoka Viwanja vya Karimjee, Dar.

Saa 4:45 asubuhi, Mwili wa marehemu Celina Kombani tayari umewasili katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar, kwa kuagwa rasmi.

Saa 5:00 asubuhi, Wasifu wa marehemu Celina Kombani inasomwa.

Saa 5:20 asubuhi, Salam za pole kwa wafiwa na Watanzania wote zinatolewa na wizara za serikali, taasisi na mashirika mbalimbali ya umma na serikali.

Saa 6:00 mchana, Viongozi mbalimbali wa serikali na waombolezaji wameanza kupita kwenye jeneza lenye mwili wa marehemu Celina Kombani, kutoa heshima za mwisho na kuuaga mwili wa marehemu,  katika Viwanja vya Karimjee, Dar.

PICHA: DENIS MTIMA/GPL

Leave A Reply