Kifaa kikubwa chenye urefu wa mita 4.5 (futi 15) na upana wa mita 1.2 ambacho hakijatambulika kimeanguka kutoka angani Kaskazini mwa Myanmar.
Kifaa hicho kiliapatikana juzi Alhamisi na kuzua taharuki miongoni mwa wakazi wa eneo hilo ambao mpaka sasa bado hawajaweza kutambua kama ni kifaa gani.
Pia kifaa kingine kilianguka juu ya paa kikiwa na maandishi ya Kichina takribani wakati mmoja na hicho kingine licha ya kutoleta madhara yeyote.
Watafiti wa mambo ya anga wameeleza kuwa huenda kifaa hicho ni mabaki ya satellite iliyorushwa na China mnamo March 11 kutokea kituo cha Jiuquan Satellite Launch Centre ili kufanya tafiti za anga.
Comments are closed.