The House of Favourite Newspapers
gunners X

Dayna Ajipakulia Minyama ya Umalkia

0

 

SEXY lady kunako Bongo Flevani, Mwanaisha Nyange ‘Dayna’, amejipakulia minyama kama yote, akidai kuwa hata akikaa nje ya gemu, hakuna wa kukalia kiti chake cha umalkia.

 

Akizungumza na OVER ZE WEEKEND Dayna amesema kuwa, gemu limekuwa na ushindani, lakini yeye kiti chake hakuna wa kukikalia maana akitoa kazi ni kazi kwelikweli.

 

“Mimi naamini hata nikikaa nje ya gemu kwa muda mrefu, narudi na ninapokelewa. Kiti changu hakuna mtu ambaye anaweza kukikalia.

 

“Kwa sasa ujanja umekuwa mwingi hata mashabiki wanaupokea huo ujanja, tofauti na zamani japo ubunifu ni mwingi ila mimi kipaji changu bado kiko moto,’’ anasema Dayna ambaye kwa sasa anatamba na Ngoma ya Homa.

STORI: HAPPYNESS MASUNGA, DAR

Leave A Reply