The House of Favourite Newspapers
gunners X

Deal Done: Dube Atua Azam FC

0

AZAM Football Club ya jijini Dar es Salaam imekamilisha usajili wa mshambuliaji wa kimataifa wa Zimbabwe, Prince Dube, kutoka  Highlanders FC ya huko.

 

Dube ambaye ni mmoja ya washambuliaji hatari Zimbabwe, akiwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya nchi hiyo cha wachezaji wa ndani, anakuja Azam  kuongeza nguvu kwenye eneo la ushambuliaji.

Benchi la ufundi la Azam  chini ya Kocha Mkuu, Aristica Cioaba, limeridhishwa  na uwezo wake kwa muda wote waliomfuatilia hadi kuamua kumsajili.

 

Huo unakuwa usajili wa saba kwenye kikosi cha Azam katika dirisha hili la usajili kwa ajili ya msimu ujao.  Wengine  ni kipa David Kissu, na beki wa kushoto Emmanuel Charles.

Wachezaji wengine walioongezwa ni kiungo mkabaji, Ally Niyonzima, viungo washambuliaji, Awesu Awesu, Ismail Aziz na Ayoub Lyanga.

Zoezi hilo litafungwa karibuni  kwa kumsajili mshambuliaji mwingine wa kimataifa.

Leave A Reply