Donald Trump: Nitawafukuza wahamiaji kwa namna ambayo haijawahi kutokea

Rais wa zamani wa Marekani, Donald Trump amesema iwapo atakuwa rais tena, atawafukuza wageni kwa namna ambayo hakijawahi kushuhudiwa katika historia ya nchi hiyo.
Trump aliyasema hayo wakati akitoa hotuba ya kuthibitisha nia ya chama chake cha Republican katika uchaguzi wa urais mwezi Novemba, katika mkutano wa chama hicho ulioingia siku ya nne na ya mwisho mjini Milwaukee.
Rais huyo wa zamani aliahidi kupunguza mfumuko wa bei na kukomesha uingiaji wa wahamiaji nchini, ambapo aliahidi kukamilisha ukuta aliouanzisha utakaotenganisha Marekani na Mexico, ambako wahamiaji mara nyingi huingilia.
Alisema atakomesha uhamiaji mara moja siku ya kwanza kwa kufunga mpaka.
Donald Trump, ambaye alitumia zaidi ya saa moja kuwasilisha hotuba yake, ambayo ilizungumzwa zaidi badala ya hotuba iliyoandikwa.

