Dude Awawakia Wanaomshambulia
STAA wa Filamu za Kibongo, Kulwa Kikumba ‘Dude’ inaonekana aliwakera baadhi ya watu baada ya kutupia picha akiwa anasali na kuamsha mashambulizi.
Akionesha naye anajua kuwaka kwa hoja kuwajibu waliomuona ameteleza, aliiambia Za Motomoto News kuwa alifanya hivyo ili kuwashawishi wengine kumcha Mungu.
“Watu huwaona wasanii kama siyo wacha Mungu, kupiga picha nikifanya ibada kinawakumbusha wafuasi wangu wenye imani kama yangu ya Kiislamu kumkumbuka Allah,”alisema Dude.
Comments are closed.