The House of Favourite Newspapers

DYNA AJAZWA KITUMBO NDII

MREMBO anayekimbiza kwenye Bongo Fleva, Mwanaisha Said ‘Dayna Nyange’ amejazwa kitumbo ndii kinachodaiwa kumpeleka puta na ndiyo sababu ya kuwa kimya kwenye muziki.

Habari ilizozipata Za Motomoto News ni kwamba mwanamama huyo ana ujauzito mkubwa ambao umekuwa ukimsumbua na mara nyingi amekuwa akijificha kwa kuwa hataki watu wengi wajue kama yupo katika hali hiyo.

“Si unajua Dayna alipata mpenzi Mzungu? Nadhani ndiye ameamua kumzalia na hataki kabisa kumtaja baba kijacho wake kwani hata marafiki zake wa karibu ametuficha,” alisema rafiki wa Dayna ambaye aliomba hifadhi ya jina lake.

 

Hivi karibuni Dayna, kwenye ukurasa wake wa Mtandao wa Kijamii wa Instagram aliweka picha yake ikimuonesha ujauzito wake ukiwa mkubwa na mashabiki wake kuanza kumpongeza kwa hatua hiyo.

Za Motomoto News ilimtafuta Dayna na kumuuliza kuhusu ujauzito wake pamoja na tetesi za kwamba anazaa na Mzungu ambapo alijibu kwa kifupi:

“Sitaki kuzungumzia mambo ya ujauzito wangu na baba kijacho maana ni maisha yangu binafsi.”

Stori: Gladness Mallya, Dar

 

Comments are closed.