The House of Favourite Newspapers

EFM Kuzindua Tamasha la Muziki Mnene Jumamosi

0
Timu ya EFM wakiwa kwenye picha ya pamoja.
KWA mara nyingine tena kituo cha redio cha Efm kinatarajia kuzindua Tamasha lake la kila mwaka lijulikanao kama muziki mnene. Tamasha hilo linatarajiwa kuzinduliwa Agosti 26 mwaka huu.
Akizungumza na wanahabari, Meneja Mkuu wa Efm na TV E, Dennis Ssebo alisema kuwa Tamasha hilo la mziki menene mwaka huu litafanyika kwa kipindi cha muda wa wiki 10 sawa na miezi 2 ambapo muziki utapigwa katika viwanja kwa mkoa wa Tanga, mbeya, Mwanza, Mtwara na katika Bar kwa mkoa wa Dar es Salaam na Pwani.

Dennis Ssebo akizungumza na wanahabari.

“Muziki mnene mwaka huu utaenda sanjari na Kampeni ya NJE NDANI ambapo vipindi vinne vitarushwa mojakwa moja katika mtaa husika kwa siku ya ijumaa, vipindi hivyo ni Joto la asubuhi, Sports headquarters,uhondo na landha 3600” alisema Ssebo.

Dennis Ssebo akizidi kueleza.

Kipindi cha funga mtaa kitakuwa kikirushwa live Siku ya Jumamosi ambayo pamoja na burudani itakayotolewa na RDjs wa efm na kutakuwa na jogging asubuhi, singeli michano, kutafuta vipaji vya wasanii wa muziki wa singeli,mpira wa miguu Kati ya timu ya efm na timu za maveterans na timu za mikoa husika. 

Wanahabari wakifuatilia tukio hilo.

Mbali na hayo pia Ssebo alieleza kuwa kutakuwa na kampeni ya ugawaji mafuta katika mikoa ya Tanga, Mtwara, Pwani na Dar ambapo vyombo vya moto vyenye stika ya masafa ha efm vitapata mafuta hayo bure.

Lengo kuu la Tamasha hilo ni kukutana na kuwashukuru wasikikizaji kwa namna walivyoipokea Efm redio na kushirikiana nao hadi sasa katika maeneo mbalimbali ya jini la Dar na mikoa mingine ambayo hivi sasa efm inasikika ikiwemo pia kujadili changamoto zinazowakabili katika maeneo yao.

Leave A Reply