The House of Favourite Newspapers

Faiza atua Bongo, roho kwatu!

KUBALI yaishe! Mwanamama wa Bongo Movies, Faiza Ally ambaye ni mzazi mwenza wa Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ ametua Bongo akitokea China na kusema sasa roho yake ni kwatu baada ya Sugu kuoa.

Faiza ameliambia Gazeti la Ijumaa Wikienda kuwa amerejea nyumbani kuendeleza nguvu ya biashara zake akiwa yuko vizuri na kusema ameshasahau maumivu aliyopitia akiwa nchini China baada ya Sugu kuoa. “Nimerudi nyumbani kwa nguvu zote na nipo sawa kabisa. Mungu amenisaidia na sasa naangalia familia na maisha yangu yajayo,” alisema Faiza kwa upole

STORI: IMELDA MTEMA,DAR

Comments are closed.