The House of Favourite Newspapers

Hamisa Mobeto Anasa Mtegoni

Mwanamitindo Hamisa Mobeto.

Mwanamitindo Hamisa Mobeto anadaiwa kunasa mtegoni baada ya ‘kuuvaa mkenge’ ulioratibiwa na hasimu wake wa siku za hivi karibuni, Zarinah Hassan ‘Zari’.

 

Kwa mujibu wa chanzo kilicho karibu na Zari, inadaiwa kuwa mjasiriamali huyo alimtumia mtu aitwaye William Bugeme ambaye pia ana ukaribu naye wa damu, ili aweze kumchukua mwanamitindo huyo, ambaye amezaa na baba wa watoto wake wawili.

 

Inadaiwa lengo la Zari ni kuona wawili hao wakiwa karibu, basi ni dhahiri kuwa ukaribu kati ya Hamisa na baba watoto wake utaisha, kwani uhusiano wa kimapenzi na William hauwezi kukubalika.

 

“Mnajua kuwa huyo Hamisa amenasa kwa Bugeme lakini hajui kuwa huo ni mpango wa Zari ili amtoe kwa baba mtoto wake, asipoangalia atatumika tu kisha atabwagwa kwani jamaa yupo kimaslahi zaidi kwa ajili ya kuokoa penzi la dada yake,” alisema Sosi huyo.

 

Kwa mujibu wa sosi huyo, picha za wawili hao wakiwa katika pozi tofauti zilinaswa hivi karibuni zikiwa zimerushwa mtandaoni.

Zarinah Hassan ‘Zari’.

Sosi huyo alikwenda mbali zaidi na kuvujisha siri ya Zari kuwa ndiye anayemtuma ndugu yake huyo ili akifanikisha kuwa naye kimapenzi itakuwa rahisi kuachana na baba wa watoto wake.

 

Hata hivyo sosi huyo alidai fungu kubwa na zuri limeandaliwa kuhakikisha Hamisa hakwepi mtego huo.

“Mwanamke ni mjanja sana sana haongei ni pesa ndio inaongea, Bugeme toka zamani anafahamiana na Hamisa sasa ameamua kumtumia huyo huyo ili kuumaliza mchezo wake kabisa, unadhani mzazi mwenzake akiona ameingia kwenye penzi na Bugeme ataendelea naye, amecheza kwelikweli,” kilitiririka chanzo.

HADITHI: SIKU ZA MWISHO ZA UHAI WANGU – SEHEMU YA 1 (Audio)

Nakuletea dakika 15 za kwanza za simulizi hii tamu ya SIKU ZA MWISHO ZA UHAI WANGU. Ukitaka kuisikiliza simulizi hii Install #GlobalPublishersApp sasa. Utasoma na kusikiliza kitabu chote kuanzia sehemu ya kwanza hadi ya mwisho bureeeee!

Android: Bofya ==>http://bit.ly/2AAQe1d
iOS: Bofya ==>http://apple.co/2Assf4M

Risasi Jumatano lilimtafuta hewani Hamisa ili azungumzie sakata hilo kama ameshalifahamu au anajipanga vipi, lakini pia kuzungumzia picha zake zinazomuonesha akiwa na kaka huyo, lakini alipopokea simu yake alisikiliza madai yote kisha akakata simu.

 

Bugeme aliwahi kutoka kimapenzi na msanii Lina Sanga na Miriam Jolwa, ‘Kabula’.

STORI: Mwandishi Wetu, Risasi Mchanganyiko

Comments are closed.