‘Hausigeli’ Anaswa Akikirushia Kichanga Kwenye Kikapu cha Takataka
Mfanyakazi wa nyumbani anashikiliwa na jeshi la polisi nchini Namibia baada ya kufanya kitendo kibaya kwa mtoto wa miezi tisa wa mwajiri wake aliyejulikana kwa jina la Annemarie Theron (31) kwa kumrushia mtoto huyo ndani ya kiakapu cha takataka kama mdoli, kitu ambacho ni kinyume na haki za binadamu.
Mfanyakazi huyo aliyetokea nchini Zimbabwe alinaswa na kamera zilizotegeshwa ndani ya nyumba hiyo na baadaye alifikishwa mahakamani siku ya Jumatatu wiki hii ambapo anaendelea kushikiliwa na jeshi hilo mpaka mwezi Oktoba mwaka huu.
Siku ya Jumapili iliyopita mama wa mtoto huyo aliposti picha ya mtoto huyo na kuandika maneno yafuatayo “My precious baby Laila Danae please know we love you endlessly and we are SO SO sorry for what you have been through!! We thank the Lord for His protection and faithfulness, that you are still alive and still such a shining ray of light to so many people – you are so loved!! Out of the depth of our hearts Johan and I want to thank EVERYONE (family, old friends, new friends and total strangers) for ALL their love, support, calls, messages and prayers during this time!!!