The House of Favourite Newspapers

SWETA LA HEMED LAZUA GUMZO

Hemed Suleiman

PENGINE hali ya hewa isiyotabirika jijini Dar es Salaam mara baridi mara joto ndiyo iliyomponza msanii Hemed Suleiman baada ya kuzuka msi­bani wakati wa jua kali akiwa na sweta na kuzua gumzo.

Za Motomoto News lilikuwa shuhuda wa tukio hilo kwenye msiba wa mtoto wa Muna uliofan­yika wikiendi iliyopita Dar, kwa kuwaona baadhi waombolezaji wakikodoa macho na kuachia wazi midomo yao huku kiulizo kikiwa: “Kulikoni huyu msanii na sweta kwenye jua kali na joto jingi?”

“Ubishoo tu huu.”

“Jamani tusihukumu yawezeka­na ana sababu za msingi za kuja na sweta.” Vi­onjo vya mijadala kutoka kwa baa­dhi waombolezaji waliofurika kumuaga mtoto huyo eneo la Viwan­ja vya Leaders Club vilisikika.

Hata hivyo baada ya shu­ghuli ya kuaga kumalizika safu hii ilimsaka Hemed lakini haikufanikiwa; lengo ni kumhoji ku­likoni sweta wakati wa jua kali, tena msibani?

 Stori : NA HAMIDA HASSAN

Comments are closed.