SWETA LA HEMED LAZUA GUMZO
PENGINE hali ya hewa isiyotabirika jijini Dar es Salaam mara baridi mara joto ndiyo iliyomponza msanii Hemed Suleiman baada ya kuzuka msibani wakati wa jua kali akiwa na sweta na kuzua gumzo.
Za Motomoto News lilikuwa shuhuda wa tukio hilo kwenye msiba wa mtoto wa Muna uliofanyika wikiendi iliyopita Dar, kwa kuwaona baadhi waombolezaji wakikodoa macho na kuachia wazi midomo yao huku kiulizo kikiwa: “Kulikoni huyu msanii na sweta kwenye jua kali na joto jingi?”
“Ubishoo tu huu.”
“Jamani tusihukumu yawezekana ana sababu za msingi za kuja na sweta.” Vionjo vya mijadala kutoka kwa baadhi waombolezaji waliofurika kumuaga mtoto huyo eneo la Viwanja vya Leaders Club vilisikika.
Hata hivyo baada ya shughuli ya kuaga kumalizika safu hii ilimsaka Hemed lakini haikufanikiwa; lengo ni kumhoji kulikoni sweta wakati wa jua kali, tena msibani?
Stori : NA HAMIDA HASSAN
Comments are closed.