The House of Favourite Newspapers

Hii Ndiyo Miji Yenye Utulivu na Amani Zaidi Duniani

0
Stuttgart.

IWAPO amani ya mawazo au akili inamaanisha kutembea kwa utulivu nyumbani ukipita kwenye miti na maua, kuwa na fedha za kutosha benki, kuwa na kazi ya uhakika, mahali bora zaidi kwa kupata amani hiyo ni katika miji ya nchini Ujerumani.

Hanover.

Utafiti mpya umeonyesha miji yenye utulivu zaidi ya mwaka 2017 kwa kutia maanani usafiri wa barabarani, usafiri wa umma, maeneo ya kupumzikia na bustani, hali za kifedha za watu wake ikiwa pamoja na viwango vya madeni, afya ya kimwili na kiakili na saa ambazo miji husika hupata mwanga wa jua kwa mwaka.

Graz.

Katika miji 150 iliyohusika, miji minne ya kwanza miongoni mwa kumi isiyokuwa na matatizo ni ile ya Ujerumani. Mji wa kusini mwa nchi hiyo wa Stuttgart ndiyo unaongoza orodha hiyo, Hanover ukishika nafasi ya tatu, Munich wa tano na Hamburg ukishika nafasi ya tisa na Graz wa Austria.

Munich.

Nchi ndogo yenye utajiri mkubwa ya Luxembour inayokaliwa na watu wasiozidi 600,000, ndiyo inashika nafasi ya pili duniani. Mji wa Bern nchini Switzerland unashika nafasi ya nne, Bordeaux (Ufaransa) wa sita, Edinburgh, Uingereza wa saba.

Bern.

Sydney, Australia (wa nane) ukiwa mji pekee usiokuwa wa Ulaya kuingia katika kumi bora wakati ambapo Seattle ndilo jiji lenye mazingira bora yasiyo ya joto nchini Marekani.

Sydney.

Utafiti huo uliofanywa na shirika moja la Uingereza liitwalo Zipjet, ulijumuisha maeneo 500 yenye kuhusisha aina 17 za mazingira mbalimbali ikiwa ni pamoja na miundombinu, viwango vya uchafuzi wa mazingira, fedha na hali za raia wake.

Kwa upande wa miji yenye matatizo na wasiwasi, Baghdad wa nchini Iraq unashika nafasi ya kwanza ukifuatiwa na Kabul (Afghanistan) ambapo Lagos nchini Nigeria barani Afrika, unashika nafasi ya tatu.

Mji miwili ya Afrika, Dakar (Senegal) na Cairo (Misri) inashika nafasi ya nne na tano katika orodha hiyo, ikifuatiwa na Tehran (Iran) inayoshika nafasi ya sita, Dhaka ya Bangladesh (nafasi ya saba) na Karachi wa Pakistan unaoshika nafasi ya nane. Miji ya New Delhi wa India na Manila (Philippines) inashika nafasi ya tisa na kumi katika orodha hiyo.

Katika utafiti huo pia palibainika kwamba Luxembourg una idadi ndogo zaidi ya watu ukifuatiwa a Kuwait City, wakati ambapo Sydney na Melbourne inayoshika nafasi ya sita na saba, maeneo yake hayana msongamano wa watu.

Kwa upande huohuo wa mazingira barani Afrika, Abidjan nchini Ivory Coast ndiyo una kiwango cha chini zaidi cha uchafuzi wa mazingira kwa upande wa sauti ambapo Antananarivo (Madagascar) una kiwango cha chini zaidi katika uchafuzi wa mazingira wa mianga wakati wa usiku, jambo linalofanya kushindikana kuonekana kwa nyota na sayari mbalimbali angani nyakati za usiku.

Leave A Reply