Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John pombe Magufuli, Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, wameungana na waombolezaji wengine kuupumzisha mwili wa aliyekuwa mwanasiasa mkongwe nchini, Mzee Kingunge, katika nyumba yake ya milele kwenye Makaburi ya Kinondoni jijini Dar.
Mbali na magufuli na Kikwete, viongozi wengine waliohudhuria mazishi hayo ni Marais Wastaafu, Benjamin Mkapa, Ali Hassan Mwinyi, Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa, Makamu wa Rais Mstaafu, Dkt. Gharib Bilali na viongozi wengine wengi wa Serikali, vyama na dini.
Comments are closed.