JUSTIN BIEBER AOMBA URAIA WA MAREKANI
MWANAMUZIKI kijana ambaye ni raia wa Canada, Justin Bieber, ametuma maombi ya kuwa raia wa Marekani, ambapo atabaki pia na uraia wake wa Canada.
Pamoja na kueleza kwake kwamba anaipenda Marekani, ni dhahiri ataipenda zaidi wakati akimwoa mchumba wake, Hailey Baldwin, ambaye ni Mmarekani.
Justina alizaliwa Ontario, Canada, lakini alihamia Atlanta, Marekani, akiwa na umri wa miaka 13 ambako ameishi na kujiendeleza kimuziki na kuwa tajiri mkubwa.
Comments are closed.