The House of Favourite Newspapers

Kagere: Wakija Okwi, Bocco Mtapata Taabu Sana

STRAIKA aliyeng’ara na Simba kwenye Kagame, Meddie Kagere amesema kwamba endapo wachezaji walioko likizo wakirejea kwenye timu hiyo akiwemo Emmanuel Okwi na John Bocco kikosi hicho kitatisha sana.

 

Kagere ametua Simba hivi karibuni akitokea Gor Mahia ya Kenya ambayo mashabiki wao mpaka leo hawaamini kilichotokea mpaka akawakimbia. Amefunga mabao manne kwenye Kagame.

 

Raia huyo wa Rwanda ambaye jana Jumamosi aliondoka kwenda kwao kukamilisha mambo yake amesema; “Unajua asilimia kubwa ya wachezaji wengi ambao tulikuwa tunacheza ndiyo mara yetu ya kwanza kuwa hapa sasa imechangia kwa namna fulani hivi kushindwa kupata kile ambacho tunakitaka kwenye Kagame.”

Meddie Kagere.

“Ninaamini kwamba wakija wachezaji wengine walio mapumziko (Okwi na Bocco) na kupata muda mzuri wa kujiandaa basi nikwambie tu hakuna ambaye atakuwa na uwezo wa kutuzuia sisi kwa msimu ujao, niwaambie tu mashabiki wasubiri,” alisema Kagere ambaye amezaliwa Uganda.

 

Kocha wa Simba, Masoud Djuma aliwapa mapumziko wachezaji waliotumika kwa asilimia kubwa kwenye ligi wakiwemo Okwi, Bocco, Aishi Manula, Haruna Niyonzima, Jonas Mkude na wengineo.

Comments are closed.