The House of Favourite Newspapers

Kibonge Sexy: Mi na Chid Benz Tumebaki Marafiki Tu!

amber-lulu-na-kibonge-sexy4

ALIYEKUWA demu wa staa wa Hip Hop, Rashid Makwiro ‘Chid Benz’, Bhoke ‘Kibonge Sexy’ kwa mara ya kwanza amefungukia uhusiano wao kuwa kwa sasa hawako kimapenzi kama zamani.

Akichonga na Global TV Online leo, Bhoke ambaye pia ni mwanamitindo na video queen mnene kuliko wote Bongo alisema, ni muda mrefu tangu awe na Chid kimapenzi na kilichobaki kwa sasa ni urafiki tu.

“Umebaki urafiki wa karibu, wa kumjulia hali na kuzungumza naye tu lakini si wapenzi tena,” alisema Kibonge Sexy.

Kibonge Sexy aliongeza tena, katika maisha yake hamuogopi mtu hivyo anavyoposti picha za nusu utupu anafanya biashara za nguo na hata kaka zake wawili wanajivunia na kutambua kitu gani anakifanya.

Kwa mahojiano kamili mazuri na matamu, usisite kutembelea mtandao wetu wa Global TV Online kwa kuingia www.globaltvtz.com

Na Andrew Carlos/GPL

Comments are closed.