The House of Favourite Newspapers

Kidoa Adaiwa Kurudia Ufuska!

                               Asha Salum ‘Kidoa’

MSANII wa filamu Bongo Asha Salum ‘Kidoa’ ambaye kwa kipindi kirefu alipoa kama maji ya mtungi kutokana na mwandani wake kumpiga ‘stop’ mambo ya kifuska ikiwemo kupiga picha za nusu utupu, amedaiwa kurejea kwenye vitendo hivyo baada ya kumwagana na jamaa huyo.

 

Kwa mujibu wa chanzo, Kidoa awali alikuwa machachari lakini alivyompata pedeshee ambaye ni kigogo wa serikali
alimpiga ‘stop’ mambo ya kifuska ikiwemo kuuza sura mitandaoni akiwa nusu utupu, pamoja na skendo kwenye vyombo vya habari.

 

Baada ya kunasa ubuyu huo, mwanahabari wetu alipomtafuta Kidoa, aliangua kicheko na kusema: “Watu wanapenda sana kufuatilia maisha yangu, najua hayo yote yameibuka baada ya kuweka picha Instagram nikiwa na nguo za ndani pekee, mavazi hayo nilikuwa nayapenda kitambo na picha zangu nyingi zilikuwa za hivyo, nikaamua tu nipumzike, si kwamba nimeachwa.”

Comments are closed.