The House of Favourite Newspapers

Kijiji India Chasherehekea Ushindi wa Kamala Marekani

0

WAKAZI wa kijiji cha   Thulasendrapuram kusini mwa  India, wamesherekea ushindi wa Makamu wa Rais Mteule wa Marekani, Kamala  Harris, ambaye ana asili ya India.   Mama wa Kamala anatoka kwenye kijiji hicho.

 

Wanakijiji hao wamekuwa wakitandika khanga na kuweka mabango na picha za Kamala kwenye barabara  na kufanya ibada kabla  ya uchaguzi ili yeye  na mgombea urais  Joe Biden washinde.

 

Kamala atakuwa mwanamke wa kwanza mwenye asili ya Mmarekani mweusi na Mhindi kushika wadhifa huo mkubwa.   Mama yake Kamala ni Mhindi  kutoka India na baba ni Mmarekani mweusi kutokea  nchini Jamaica.

 

Haris anakuwa mtu wa kwanza Mu-Asia kuwa Makamu wa Rais wa Marekani.  Mama yake alizaliwa India lakini baadaye akahamia Marekani kwenda kusoma akiwa na miaka 19 .

 

Leave A Reply