The House of Favourite Newspapers

Kikwete Ampa Tano Lowassa Kurejea CCM

Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Dkt Jakaya Kikwete amempongeza Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kwa uamuzi wake wa kurejea Chama cha Mapinduzi (CCM).

 

Lowassa alijiunga CHADEMA Julai 2015 baada ya jina lake kuenguliwa kwenye mchakato wa kutafuta mgombea wa urais ndani ya CCM.

 

“Karibu tena nyumbani, Hongera kwa uamuzi wa busara,” ameandika Dkt. Kikwete kwenye ukurasa wake wa mtandao wa Twitter.

Lowassa alitangaza hapo jana kurejea CCM katika ofisi ndogo za chama hicho zilizopo Lumumba Dar es Salaam na kupokelewa na Mwenyekiti wa CCM taifa, Rais John Magufuli.

 

 

Comments are closed.