The House of Favourite Newspapers

Kisa Lissu… Mchungaji Msigwa, Amvagaa Spika Ndugai

0
Mchungaji Peter Msigwa.

MBUNGE wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa amemjia juu Spika wa Bunge, Job Ndugai akimtaka kuacha kudanganya kuwa ndege iliyomsafirisha Tundu Lissu ilikodiwa na mbunge wa CCM.

Spika Ndugai Amjibu Lema Kuhusu Bunge na Serikali Kutomsaidia Lissu


Maelezo ya Mchungaji Msigwa yamekuja saa chache baada ya Spika Ndugai kueleza bungeni kuwa mbunge wa CCM ndiye aliyeagiza ndege kutoka Nairobi kwa gharama za dola za Marekani 9,200 kumsaidia Lissu halafu atakuja kurudishiwa.
Baada ya maelezo hayo Msigwa ambaye yuko na Lissu kwenye matibabu jijini Nairobi ameandika, “Spika Ndugai muogope Mungu, usilete utani katika maisha ya Mh Lissu, umeliongopea Bunge na umma, gharama zote za ndege zimelipwa na Chadema na Watanzania. The parliament deserve better than you!

Ukweli Kuhusu Ndege Iliyompeleka Lissu Nairobi na Deni linalodaiwa

Leave A Reply