MBUNGE wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa amemjia juu Spika wa Bunge, Job Ndugai akimtaka kuacha kudanganya kuwa ndege iliyomsafirisha Tundu Lissu ilikodiwa na mbunge wa CCM.
Spika Ndugai Amjibu Lema Kuhusu Bunge na Serikali Kutomsaidia Lissu
Maelezo ya Mchungaji Msigwa yamekuja saa chache baada ya Spika Ndugai kueleza bungeni kuwa mbunge wa CCM ndiye aliyeagiza ndege kutoka Nairobi kwa gharama za dola za Marekani 9,200 kumsaidia Lissu halafu atakuja kurudishiwa.