WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, amemtaka Mkuu wa Magereza nchini, Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Martin Kasike, kuweka na kumpelekea mikakati ya kuhakikisha wafungwa wanajilisha kwa kufanya kazi badala ya kulishwa kwa fedha za serikali.
Ameonya pia kwamba iwapo mfungwa atakamatwa na simu gerezani, mkuu wa gereza husika atakuwa amepoteza sifa za kazi yake.
Lugola ameyasema hayo leo alipozungumza na vyombo vya habari na kusisitiza wito wa Rais John Magufuli wa kutaka wafungwa wajitegemee kwa chakula na kuhakikisha wafungwa hawaingizi simu gerezani.
Comments are closed.