The House of Favourite Newspapers

MAKAMBA AKABIDHI OFISI KWA GEORGE SIMBACHAWENE

Aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. January Makamba akikabidhi Ofisi kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Boniface Simbachawene katika Ofisi ndogo ya Makamu wa Rais jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Boniface Simbachawene akimsindikiza Mhe. January Makamba mara baada ya kukamilika kwa hafla ya makabidhiano ya Ofisi katika Ofisi ndogo Dar es Salaam. Katikati ni Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Mussa Sima.
Picha ya pamoja baada ya makabidhiano ya Ofisi: Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Boniface Simbachawene (kulia) Mhe. January Makamba na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mussa Sima.

Aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. January Makamba leo Jumatano Julai 24, 2018 amekikabidhi Ofisi kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Boniface Simbachawene katika Ofisi ndogo ya Makamu wa Rais jijini Dar es Salaam.

Comments are closed.