The House of Favourite Newspapers

Makonda akagua patakapo jengwa Hospitali ya Ubungo

Siku chache baada ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli kutoa fedha kiasi cha Shilingi Bilioni 1.5 kwaajili ya Ujenzi wa Hospital ya Wilaya ya Ubungo, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda leo ametembelea na kukagua eneo itakapojengwa hospital hiyo na kuwaekekeza JKT kuhakikisha wanafanya kazi usiku na Mchana na kukabidhi jengo ndani ya Miezi mitatu kuanzia leo ili wananchi wa wilaya hiyo wapate huduma Bora za Afya.

RC Makonda amesema Hospital hiyo inajengwa eneo la Kimara Baruti kwenye eneo lenye ukubwa wa Hekari 5.5 ambapo amemshukuru Rais Magufuli Kwa moyo Wa Upendo anaoendelea kuonyesha kwa Wakazi wa Dar es salaam na Wilaya ya Ubungo.

Aidha RC Makonda amesema kuwa maandalizi yote ya ujenzi yamekamikika na kazi ujenzi itaanza rasmi kesho huku akibainisha kuwa kukamikika kwa Hospital hiyo kutasaidia kwa kiasi kikubwa kumaliza changamoto za Afya Wilayani humo.

 

Itakumbukwa Juzi October 26 wakati wa hafla ya Kupokea ndege ya 8 Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda alitumia hafla hiyo kuwasilisha kilio cha wakazi wa Ubungo juu ya kukosekana kwa hospital ya wilaya ya Ubungo ambapo Rais Magufuli alipokea kwa mikono miwili ombi hilo na Kumuelekeza Waziri wa TAMISEMI kutoa fedha hizo na hatimae leo utekelezaji wa ujenzi unaanza.

 Mattukio katika Picha:

Imeandaliwa na Neema Adrian/GPL

Comments are closed.