The House of Favourite Newspapers

Man Fongo Adondoka Juu ya Paa

0
Amani Fongo ‘Man Fongo’.

MSANII wa muziki wa Singeli nchini, Amani Fongo ‘Man Fongo’ mwishoni mwa wiki iliyopita alinusurika kifo baada ya kutereza juu ya paa la nyumba wakati akiweka balbu ya umeme.

Akisimulia mkasa huo kwa Risasi Vibes, Man Fongo alisema tukio hilo lilitokea Sinza jijini Dar alikohamia ambako alikuwa akisimamia mafundi waliokuwa wakiifanyia ukarabati nyumba hiyo, ambapo alipoanguka, mkono wake mmoja uliingia katika chuma kimoja cha geti na kum-pasua kiasi cha kutokezea upande wa pili.

“Nashu-kuru kwa sasa naendelea vizuri baada ya kupatiwa matibabu, kiukweli sijui ilikuwaje mpaka nikatereza kwani nilishtukia nimedondoka na kuumia, maumivu niliyoyapata siwezi hata kuyaelezea kwa kweli,” alisema Man Fongo.

Stori: Irene Mnyitafu| Risasi Mchanganyiko

Usipitwe na Matukio, Install ===>Global Publishers App

Man Fongo Azinguana na Meneja Wake, Anyang’anywa ALTEEZA Anunua VOLKSWAGEN

Leave A Reply