Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Eng. Hamad Yussuf Masauni ametangaza kuwa, Jeshi la Polisi linawaska watuhumiwa 16 wa mauaji ambayo yamekuwa yakiendelea kufanyika katika maeneo ya Kibiti, Mkuranga na Rufiji Mkoani Pwani kwa muda mrefu sasa.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Masauni amesema kuwa watuhumiwa hao wanafahamika na tayari jeshi la polisi lina picha za watuhumiwa wote ambao wanasakwa.
“Nchi yetu ipo katika changamoto ya matukio katika maeneo ya Kibiti na Rufiji, ambapo matukio haya wakati mwingine yanaripotiwa ndivyo sivyo na vyombo vya habari na kusababisha hofu kwa wananchi. Sisi kama serikali lazima tuwatoe hofu wananchi wetu. Tuwaombe wanahabari mfikishe ujumbe sahihi zaidi.
“Jana tulifanikiwa kuwadhibiti wahalifu wawili kabla hawajatekeleza uhalifu wao, kwa hiyo jeshi letu linafanya kazi vizuri sana. Suala la kumaliza uhalifu wa Kibiti ni la lazima wala sio la mjadala tena.
“Maandalizi ya mkoa Mpya wa Kipolisi wa Rufiji yamekamilika na Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo tayari ameshateuliwa,” alisema Masauni.
#WaziriMasauni: Muda si mrefu hayo mauaji ya Kibiti yatakoma.
— Global Publishers (@GlobalHabari) June 30, 2017
#NaibuWaziriMasauni: Mkoa wa Kipolisi Rufiji umeshakamilika na RPC wa mkoa huo tayari amekwisha chaguliwa, hivi karibuni atatangazwa. pic.twitter.com/k3XBoQI8Q2
— Global Publishers (@GlobalHabari) June 30, 2017
#Masauni: Kuna watu 16 tunawatafuta hasa kwenye haya mauaji ya Kibiti, tunawafahamu na picha zao tunazo.
— Global Publishers (@GlobalHabari) June 30, 2017
#IGP_SIRRO: Juzi hapa tumeua majambazi wanne, kwa hiyo tunafanya kazi vizuri na kwa makini.
— Global Publishers (@GlobalHabari) June 30, 2017
#IGP_SIRRO: Suala la ulinzi shirikishi ni la muhimu kwa mkoa wa Dar es Salaam.
— Global Publishers (@GlobalHabari) June 30, 2017
#IGP_SIRRO: Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Rufiji ni Kamishna Onesmo Lyanga. Wananchi wa Rufiji wampe ushirikiano.
— Global Publishers (@GlobalHabari) June 30, 2017
#IGP_SIRRO: Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Rufiji ni Kamishna Onesmo Lyanga. Wananchi wa Rufiji wampe ushirikiano.
— Global Publishers (@GlobalHabari) June 30, 2017
‘Matatizo ya maeneo ya Kibiti hayawezi kuisha kwa nguvu ya Polisi pekee, yataisha kwa ushirikiano na wananchi wa maeneo hayo’ – IGP Sirro pic.twitter.com/l4T8hFBxFx
— Global Publishers (@GlobalHabari) June 30, 2017
PICHA ZOTE NA DENIS MTIMA | GLOBAL TV ONLINE
=====
TAZAMA VIDEO WAKIFUNGUKA HAPA