The House of Favourite Newspapers

Mastaa Walioitwa Mama 2017

Mwanamitindo wa kimataifa, Hamisa Mobeto akiwa na mwanae.

MWAKA 2017 ndiyo huo unayoyoma na zimebaki siku kumi tu kuingia mwaka 2018. Mwaka 2007, mengi yametokea kwa kila mtu katika maisha yake ya kawaida.

 

Wapo waliofanikiwa, waliofeli na wapendwa wetu wengine walitutoka kabisa. Kama ilivyo kwenye maisha ya kawaida kuwa na mengi yaliyotokea, vivyo hivyo kwenye ulimwengu wa burudani. Ukiachana na kiki zilizotikisa, matukio ya kuvutia na mengine mengi mazuri na mabaya tumeyashuhudia kwa staa mmojammoja.Miongoni mwa hayo mazuri ni kwa baadhi ya mastaa wa kike ambao walihabatika kuitwa mama kama ifuatavyo;

Muigizaji Faiza Ally akiwa na mtoto wake Lil Junior

MAMA KAIRO (HAPPINESS MILLEN MAGESE):

Mwishoni mwa Julai, mwaka huu, baada ya kutafuta mtoto kwa muda mrefu, mwanamitindo maarufu wa kimataifa, Happiness Millen Magese ‘Ladiva Millen’ alijibiwa kilio chake na Mungu wake. Millen alijaliwa mtoto wa kiume aliyempa jina la Prince Kairo Michael Magese. Kupitia ukurasa wake wa Mtandao wa Instagram, Millen alionesha furaha yake kwa kuandika ujumbe matata ambapo pia alifafanua jina la mtoto
wake huyo la Kairo kwamba, linamaanisha ‘utukufu kwa Mungu.’

 

MAMA JADEN (CHUCHU HANS):

Uhusiano wake na muigizaji Vincent Kigosi ‘Ray’ ulianza kama siri. Ghafla, muigizaji Chuchu Hans ni mjamzito. Baadaye mambo yalikuwa wazi hasa Mwezi Januari, Chuchu alipojifungua mtoto wa kiume ambaye yeye na mpenzi wake, Ray walimpa jina la Jaden.

 

MAMA GOLD (AIKA):

Baada ya kudumu kwenye uhusiano kwa zaidi ya miaka nane, Aika na mpenzi wake, Nahreel, mwanzoni mwa Mwezi Desemba walibahatika kupata mtoto wa kiume ambaye
walimpa jina la Gold.

 

MAMA PRINCE ABDUL (HAMISA MOBETO);

Mwanamitindo wa kimataifa, Hamisa Mobeto naye anaingia kwenye orodha hii baada ya Mwezi Agosti, mwaka huu kupata mtoto wa kiume aliyempa jina la Prince Abdul. Kwa Hamisa, huyu ni mtoto wa pili kufuatia awali kupata mtoto wa kike aitwaye Fantas.

 

MAMA CLARIBELL (ESHA BUHETI);

Wakati ikiwa imepita siku moja tu baada ya mwanamitindo Hamisa Mobeto kupata mtoto wa kiume, muigizaji Esha Buheti naye alibahatika kupata mtoto
wa kike ambaye alimpa jina la Claribell. Kama ilivyo kwa Hamisa, kwa Esha pia huyo naye ni mtoto wake wa pili. Mtoto wa kwanza anaitwa Clarisa.

 

MAMA LIL JUNIOR (FAIZA ALLY);

Muigizaji Faiza Ally naye yumo kwenye orodha hii. Mwaka 2017, kwake umekuwa na mafanikio mengi ikiwemo kupata mtoto wa kiume ambaye amemuita Lil Junior. Naye ni mtoto wake wa pili baada ya Sasha aliyezaa na Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’. Wengine waliopata watoto kwa mwaka 2017 ni pamoja na staa wa Bongo Fleva, Estarlina Sanga ‘Linah’ Khadija Nito na muigizaji Welu Sengo.

Makala: BONIPHACE NGUMIJE

Comments are closed.