The House of Favourite Newspapers

MAYWHEATHER AFANYA KUFURU NYINGINE YA BILIONI 12.1

Bondia marufu, ‘Floyd Maywheather’ amefanya kufuru ya pesa baada ya kufanya shopping ya kununua Bangili, Pete pamoja na Mkufu kwa Dola Milioni 5.3 (Tsh Bilioni 12.1) Novemba 14, 2018 wiki iliyopita.

 

Maywheather aliumia Dola Milioni 2.3 kununua pete ya ragi ya njano, Dola 2.5 kununua bangili ya Almasi na Dola Laki 5 alinunulia saa tatu na mkufu.

 

Bondia huyo maarufu imekuwa kawaida yake kutumia pesa zake kununua vitu vya ghali zaidi duniani, yakiwemo magari, saa, nyumba, nguo, mikufu, viatu na vingine vingi, anategemea kuingia kwenye mechi mwisho wa mwaka huu na bondia wa Japan, ‘Tenshin Nasukawa’.

Comments are closed.