The House of Favourite Newspapers

Mke wa Majuto Akesha Akimuombea Mumewe

 

MKE wa mchekeshaji maarufu Bongo, Amri Athuman ‘Majuto’, Aisha Yusuf amesema kuwa siku za hivi karibuni alipoanza kuugua tena mumewe amekuwa akikesha na kumuombea arudi katika hali ya kawaida kwani anapoumwa vitu vyote vinalala.

 

Akichonga na gazeti hili mke huyo alisema mume wake ni mcheshi sana na ni mtu anayeifanya familia kuwa na furaha kila wakati sasa anapokuwa mgonjwa nyumba inakuwa haina amani kabisa na hata watoto ambao amezoea kucheza nao wanapoa.

 

“Kila siku dua zangu ni kwa mume wangu maana ndiyo nguzo katika familia yetu na ni mtu mcheshi sana kwa familia hivyo namuombea sana apone maana ndiye furaha yangu,“ alisema mke wa Majuto.

 

Stori: Imelda Mtema, Dar

Comments are closed.