The House of Favourite Newspapers

MKUU WA SHULE MWENYEHERI ANUARITE ATEMBELEA OFISI ZA GLOBAL PUBLISHERS

Mhariri wa Gazeti la Amani wa Kampuni ya Global Publishers, Erick Evarist akiwaonyesha bango lenye magazeti yanayozalishwa na kampuni hiyo.
Mwanafunzi  ambaye ni mhitimu wa kidato cha sita, Prosper Nyambe (katikati) akisalimiana na Mhariri wa Gazeti la Ijumaa Wikienda, Sifael Paul. Kushoto ni Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Mwenyeheri Anuarite, Carlos Mgumba.
Erick Evarist akiwatambulisha kwa Mhariri wa Gazeti la Championi linalotoka Jumatatu, Ezekiel Kitula (kulia wa kwanza)
Wakijionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na upande wa wasanifu kurasa kutoka kwa Shafii Mohammed (aliyekaa).
Mkuu  wa Shule ya Sekondari ya Mwenyeheri Anuarite, Carlos Mgumba (wa pili kushoto) akisalimiana na Mkuu wa Kitengo cha Global TV Online, James Range.
Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Mwenyeheri Anuarite iliyopo Kimara jijini Dar es Salaam, Carlos Mgumba akifanya mahojiano na Global TV Online.

MKUU  wa Shule ya Sekondari ya Mwenyeheri Anuarite iliyopo Kimara jijini Dar es Salaam, Carlos Mgumba hivi karibuni alitembelea ofisi za Kampuni ya Global Publishers Ltd na kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa hapo.

 

Akiwa ofisini hapo, alisema amefurahi kujionea kazi zinazofanywa ambapo  alifarijika kuona kampuni hiyo ikiwa na vijana wengi wakifanya kazi hapo ambao ndiyo nguvu kazi ya taifa la kesho.

 

Mgumba aliweza kutembelea idara mbalimbali za magazeti Pendwa ambayo ni Ijumaa Wikienda, Uwazi, Risasi, Amani, Ijumaa, Risasi Jumamosi na gazeti la Michezo la Championi na kubadilishana mawazo na wahariri pamoja na waandishi wa magazeti hayo ikiwa ni moja ya  kukuza mahusiano mema. 

 

Aidha katika matembezi yake aliambatana na mwanafunzi wake ambaye ni mhitimu wa kidato cha sita, Prosper Nyambe ambaye aliweza kufanya mahojiano kupitia Global TV Online juu ya kipaji chake alichonacho.

 

Mkuu huyo  alisema   shule yake inawapatia wanafunzi wake elimu ya ziada ya kuelewa namna ambavyo  wanaweza kujikwamua kiuchumi wamalizapo masomo yao kupitia midahalo mbalimbali ambazo zimepelekea kuibua kipaji cha mwanafunzi huyo.

 

Na Denis Mtima/GPL

Comments are closed.