Mmh! Amber Rose ni Kweli au Unatudanganya tu
HIVI ni kweli ama? Huku ikiwa imepita miezi sita tangu mwaka uingie, mwanamitindo mwenye jina kubwa aliyekuwa mpenzi wa mwanamuziki Wiz Khalifa, Amber Rose ameibuka katika akaunti yake kwenye Mtandao wa Kijamii wa Twitter na kudai kwamba tangu mwaka 2017 uingie hajawahi kulala na mwanaume yeyote yule.
Kauli hiyo kutoka kwa mwanamama huyo mwenye mtoto mmoja aitwaye Sebastian imezua mijadala mitandaoni huku wengine wakihoji kama anachokisema ni kweli au amedanganya ilimradi awe na cha kuongea kwani kwa kipindi kirefu amekuwa hasikiki kama ilivyokuwa zamani.