SERIKALi imekabidhi ndege yake aina ya Fokker 50 kwa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) kwa ajili ya kubeba abiria wa kawaida kama ilivyoagizwa na Rais John Magufuli.
Hafla fupi ya kukabidhi ndege hiyo imefanyika leo, Aprili 1, 2019, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.
Fokker 50 ilikuwa ikibeba viongozi mbalimbali lakini Rais Magufuli aliagiza ikabidhiwe kwa ATCL ili kuongeza nguvu na kuendelea kulikuza shirika hilo ambalo amedhamiria kuliboresha.
Comments are closed.