The House of Favourite Newspapers

NUH MZIWANDA AFUNGUKIA TETESI ZA KURUDIANA NA SHILOLE

MSANII wa Bongo fleva Naftal Mlawa ‘Nuh Mziwanda’, amefungukia tetesi za kurudiana na msanii mwenzake wa ambaye pia alikuwa mepenzi wake wa zamani kabla ya kila mtu kushika hamsini zake Zuwena Mohamed ‘Shilole’ kwa kuweka wazi kwamba hana wazo wala hisia zozote za kurudiana na msanii huyo kwa siku za hivi karibuni.

Akipiga stori na Mikito Nusunusu Nuh mziwanda alisema kwamba amekuwa akizisikia tetesi za uwepo wa penzi la chinichini kati yake na Shilole licha ya kwamba mwanamke huyo ni mke wa mtu.

“Siwezi kurudiana na Shilole hata iweje, mimi kurudiana na shilole ni stori tu ambazo watu wanazusha,ukweli siwezi kumrudia mtu huyo. Na sivutiwi kuzungumzia habari zake kwa sasa kwakuwa anamaisha yake ya ndoa takatifu, si vizuri kumwongelea kwa sasa. Siwezi kurudiana na Shishi” alisema Nuh Mziwanda

Comments are closed.