The House of Favourite Newspapers

Picha za Utupu Kumkimbiza Bongo Pretty Kind

Suzan Michael ‘Pretty Kind’

MSANII wa filamu Bongo, Suzan Michael ‘Pretty Kind’ amepanga kutimkia nchini India alipokuwa anaishi siku chache zilizopita kwa bwana’ke, baada ya kupigwa kufuli na Naibu Waziri wa Habari Sanaa na Michezo, Juliana Shonza kutokana na kuweka picha zisizo na maadili mtandaoni (nusu utupu).

Suzan Michael ‘Pretty Kind’ akiwa nchini India.

Kwa mujibu wa chanzo chetu, baada ya mwanadada huyo kupewa agizo hilo na serikali alipagawa na kuona haoni faida ya kuendelea kuwepo Bongo kwa kipindi hicho kwa kuhofia kuchekwa na watu na kuona bora arudi India kwa mwandani wake aliyekuwa akiishi naye miaka ya nyuma.

 

Alipotafutwa na paparazi wetu, Pretty alifunguka: “Ni kweli najiandaa ‘soon’ naenda India, maana masharti niliyopewa ni magumu mno kuambiwa hata picha nisiweke mtandaoni imeniuma sana, ili nitii vizuri hili agizo nimeona bora nisiwepo hapa nchini, adhabu ikiisha nitarudi.”

Stori: Mayasa Mariwata

Comments are closed.