Rais Samia Aelekea Senegal Kuhudhuria Mkutano Jumuiya ya Maendeleo Afrika-Picha
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ameondoka nchini leo Julai 6, 2022 kuelekea Dakar, nchini Senegal kuhudhuria Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kimataifa (IDA Summit for Africa).
Katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere mkoani Dar es Salaam, Rais Samia ameagwa na viongozi mbalimbali akiwemo Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango.