The House of Favourite Newspapers

Rais Samia Atoa Rai kwa Wizara ya Kilimo Kuanzisha Kilimo cha Kisasa (Picha +Video)

0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Viongozi mbalimbali pamoja na wananchi katika Sherehe za ufunguzi wa barabara ya Tabora-Koga-Mpanda 342.9 km zilizofanyika Sikonge Mkoani Tabora tarehe 18 Mei, 2022.

 

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ametoa rai kwa Wizara ya Kilimo kuanzisha na kuendeleza kilimo na ufugaji wa kisasa ikiwa ni sambamba na kuweka mikakati ya ujenzi wa viwanda vidogovidogo hasa katika mikoa ya Tabora na Katavi.

 

Rais Samia ameyasema hayo wakati anafungua Barabara ya Tabora- Koga-Mpanda yenye urefu wa Kilomita 342.9 iliyojengwa kwa kiwango cha lami.

Rais Samiaakiwa na Meneja Mkaazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) nchini Tanzania Dkt. Patricia Laverley wakati akikata utepe kuashiria ufunguzi wa barabara ya Tabora-Koga-Mpanda 342.9 km uliofanyika Sikonge Mkoani Tabora tarehe 18 Mei, 2022. Wengine katika picha ni Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa, Mkuu wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Buriani, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) Mhandisi Rogatus Mativila pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tabora Mzee Hassan Mwakasubi

 

Rais Samia amesisitiza kuwa ujenzi wa miundombinu hiyo utawezesha kukua kwa uchumi wa mikoa husika lakini pia taifa kwa ujumla na itasaidia zaidi katika upatikanaji wa mazao yanayozalishwa kutoka mashambani ambayo kwa kiwango kikubwa mikoa hiyo imekuwa ikijitahidi katika uzalishaji.

 

Rais Samia pia amegusia kuwa barabara hiyo imejengwa kwa ushirikiano wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Benki ya Maendeleo ya Afrika kwa gharama ya shilingi Bilioni 473.879

Rais Samia pamoja na Meneja Mkaazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB nchini Tanzania Dkt. Patricia Laverley wakifungua rasmi barabara ya Tabora-Koga-Mpanda 342.9 km Sikonge Mkoani Tabora tarehe 18 Mei, 2022. Wengine katika picha ni Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa, Mkuu wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Buriani, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini TANROADS Mhandisi Rogatus Mativila pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Tabora Mzee Hassan Mwakasubi
Rais Samia akiwapungia mkono Wananchi waliojipanga kando kando ya barabara ya Tabora Mpanda katika eneo la Sikonge mara baada ya kuifungua barabara hiyo, wa kwanza kulia ni Meneja Mkaazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) nchini Tanzania Dkt. Patricia Laverley.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiagana na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tabora Mzee Hassan Mwakasubi pamoja na Viongozi Wengine mara baada ya sherehe za ufunguzi wa barabara ya Tabora-Koga-Mpanda 342.9 km uliofanyika Sikonge Mkoani Tabora tarehe 18 Mei, 2022.
Viongozi mbalimbali pamoja na Wananchi wa Sikonge mkoani Tabora wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan wakati akiwahutubia katika Sherehe za ufunguzi wa barabara ya Tabora-Koga-Mpanda 342.9 km uliofanyika Sikonge Mkoani Tabora tarehe 18 Mei, 2022.

Leave A Reply