The House of Favourite Newspapers

Rais Samia Azungumza na Kamala Harris, Makamu wa Rais wa Marekani – (Picha +Video)

0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiwa na Mwenyeji wake Makamu wa Rais wa Marekani, Kamala Harris wakati wakizungumza na Wanahabari katika Ikulu ya Marekani White House Washington tarehe 15 Aprili, 2022.

 

RAIS Samia Suluhu Hassan Aprili 15, 2022 amekutana kwa mazungumzo na Makamu wa Rais wa Marekani Kamala Harris karibu na Ikulu ya Marekani ambapo ameliomba taifa hilo kubwa kuongeza mashirikiano ya sekta yake binafsi nchini Tanzania.

“Ombi langu la pekee hapa ni kuitaka serikali ya Marekani kuhimiza zaidi sekta binafsi kufanya kazi nasi,” alimwambia Kamala jijini Washington DC siku ya Ijumaa. “

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akizungumza na Makamu wa Rais wa Marekani Kamala Harris mara baada ya kuwasili Ofisini kwake katika Ikulu ya Marekani White House Washington leo tarehe 15 Aprili, 2022.

“Serikali yangu ingependa kuona uhusiano wetu ukikua zaidi na kuimarishwa hadi kufikia kiwango cha juu.”

Mkutano huo wa kihistoria baina ya viongozi hao umekuwa wa kipekee ukiwaleta pamoja Rais Samia, Mwanamke wa kwanza kuongoza Taifa la Tanzania na Kamala Mwanamke Mweusi wa Kwanza kushika wadhifa wa Makamu wa Rais kwa Taifa hilo kubwa duniani.

Rais Samia akizungumza jambo na Mwenyeji wake Makamu wa Rais wa Marekani Kamala Harris wakati akiangalia mandhari ya Majengo ya Ofisi za Ikulu ya Marekani mara baada ya kuzungumza na Wanahabari katika Ikulu hiyo ya White House Washington  tarehe 15 Aprili, 2022.

 

Kabla ya mkutano wao, Kamala aliwaeleza waandishi wa habari kuwa majadiliano kati yake na Rais Samia yatahusu kuimarisha demokrasia, uwekezaji na ukuaji wa uchumi, na afya.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiagana na Makamu wa Rais wa Marekani, Kamala Harris mara baada ya mazungumzo na Ujumbe wa Tanzania katika Ikulu ya Marekani Whitehouse nchini Marekani tarehe 15 Aprili, 2022.


“Utawala wetu umejitolea sana kuimarisha uhusiano nchini Tanzania na nchi za Afrika kwa ujumla,” Harris alisema. “Hili limekuwa eneo la umakini na kipaumbele kwa rais [Joe Biden] na kwangu.”

Hii ni mara ya pili kwa Rais Samia kufanya ziara nchini Marekani. Mara yake ya kwanza ilikuwa pale alipo hotubia kikao cha 76 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA) mwezi Septemba 2021.

PICHA NA IKULU

Leave A Reply