ROMA AGAWA MAGAZETI BURE KWA WAKAZI WA MBAGALA
Mwanamuziki wa Hip Hop Bongo, Ibrahimu Musa ‘Roma Mkatoliki’ leo amepita mitaa mbalimbali ya Mbagala akigawa Magazeti ya Risasi Mchanganyiko pamoja na Championi Jumatano, ambayo yana kuponi kushinda Pikipiki.
Jumapili hii kuanzia saa nane mchana, mkali huyo wa ngoma ya Zimbabwe, ataamsha popo pamoja Man Fongo na Juma Nature kwenye tamasha ba’b kubwa la bure la kuwashukuru Watanzania lijulikanalo kama Tusua Maisha na Global litakalofanyika kwenye Uwanja wa Taifa wa Burudani wa Dar Live.
(PICHA: RICHARD BUKOS | GPL)
Comments are closed.